
Kura ya maoni yafanyika katika majimbo Ukraine
Katika majimbo ya Donetsk na
Luhansk yaliyoko mashariki mwa Ukraine , raia wamepiga kura katika
uchaguzi wa kura za maoni usio rasmi ulioandaliwa na makundi yanayounga
mkono Urusi .
Waandalizi wa uchaguzi huo katika jimbo la
Donetsk wametangaza kile walichosema ni matokeo ya mwisho saa chache
kabla ya kufunga vituo vya kupigia kura.Wanasema karibu asilimia tisini ya watu wamepiga kura ya ndio kuunga mkono azma ya kujitawala katika uchaguzi ulioshirikisha asilimia sabini na tano ya wapiga kura.
Wapiganaji waliifyatua risasi katika eneo moja ambapo kundi lingine la wapiganaji wanaounga mkoni serikali waliripotiwa kufunga baadhi ya vituo vya kupigia kura.
Hili lilikua tukio la kipekee.
Kwa jumla shuguli ya upigaji kura katika maeneo mengi ya Donetsk na Luhansk ambayo yako mpakani mwa Ukraine na Urusi.
Hatahivyo waandishi wa BBC waliotembelea baadhi ya vituo wanasema shughuli yenyewe haikufikia viwango vya kimataifa .
Hakukua na orodha ya wapigaji kura na watu walipewa makaratasi ya upigaji kura baada ya kutoa vitambulisho.

Kura ya maoni yafanyika katika majimbo Ukraine
Serikali ya Ukraine imeitaja kura hiyo kama usiyohalali lakini Kamishna wa uchaguzi Roman Lyagin amesesitiza kuwa matokeo hayo ni sauti ya raia wenye haki ya kusikilizwa.
Kura hiyo ya maoni imefanyika licha ya wito wa Rais wa Urusi Vladmir Putin kutaka iahirishwe.
Viongozi wa nchi za Magaribi wanamlaumu kwa kusababisha mgawanyiko nchini Ukraine.
Muungano wa Ulaya umesema kura hiyo ya maoni sio halali na unajiandaa kuendelea kuishinikiza Urusi kwa kuongeza vikwazo vilivyowekwa baada ya Moscow kulitwaa eneo la Ukraine la Crimea.
ARUSO